Bingwa mtetezi wa French Open, Carlos Alcaraz, alionesha ubora wa hali ya juu kwa kumshinda Tommy Paul, na kufuzu kuingia hatua ya nusu fainali katika mashindano ya Roland Garros.
Carlos Alcaraz ambaye ni mchezaji namba mbili kwa ubora duniani, alihitaji dakika 53 pekee kupata uongozi wa seti mbili kwa sifuri (2-0), akipoteza mchezo mmoja tu katika kipindi hicho.
Mmarekani Paul alionyesha upinzani mkubwa zaidi katika seti ya tatu, ingawa Alcaraz, mwenye umri wa miaka 22, alionyesha ubora wake baada ya kumdhibiti mpinzani wake huyo na kupata uongozi wa 5-4 kabla ya kukamilisha ushindi wa 6-0, 6-1, 6-4.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa.
Mhisipania huyo sasa atakutana na Lorenzo Musetti mwenye umri wa miaka 23 katika hatua ya nusu fainali siku ya Jumapili.



