Tokyo Marathon 2021 Yahairishwa.


Mbio za Tokyo Marathon zimeahirishwa hadi Michezo ya Olimpiki ya Tokyo iliyoratibiwa upya kwa sababu ya corona, itapangwa upya hapo mwakani.

Hii ni kwa mujibu wa watayarishaji ambao wameshikilia kwamba ujio wa janga la corona utaendelea kuathiri kalenda za michezo mbalimbali kwa kipindi cha misimu kadhaa ijayo.

Awali, mashindano ya Tokyo Marathon yalikuwa yafanyike Machi 7, 2021 na yalitarajiwa kuwakutanisha zaidi ya wanariadha 38,000 duniani kote.

 

Tokyo Marathon 2021 Yahairishwa.

Hata hivyo, uchache wa watu wanaokubaliwa kuingia nchini Japan na ugumu wa kanuni zilizowekwa ili kudhibiti maambukizi zaidi ya corona sasa umechangia michezo hiyo kupangwa upya hadi Oktoba 17, 2021.

Haya ni kwa mujibu wa watarishaji na wadhamini wa mbio hizo, Tokyo Marathon Foundation.

Marathon kubwa duniani, isipokuwa ya London iliyojumuisha wanariadha wakubwa mnamo Oktoba 4, ziliahirishwa au kufutuliwa mbali kabisa kwa sababu ya corona.

Mbio za Tokyo Marathon mwaka huu wa 2020 zilifanyika Machi na zikihusisha wanariadha wachache zaidi katika historia – 200.

 

Tokyo Marathon 2021 Yahairishwa.

Kwa mujibu wa watayarishaji, hatua ya kuruhusu mashindano ya mwaka ujao kufanyika baada ya Olimpiki itawapa wanariadha nafasi nzuri zaidi ya kushiriki mbio hizo kwa wingi ila idadi ya watakaoshiriki bado haijaamuliwa.

Olimpiki za Tokyo, Japan zilizoahirishwa mwaka huu sasa zitaandaliwa mnamo Julai 23, 2021. Hata hivyo, tarehe hiyo huenda ikabadilishwa tena kutegemea viwango vya maambukizi na hali itakayokuwa imezuliwa na corona duniani kufikia wakati huo.


Weka Pesa kwa Airtel Money!

Sasa unaweza kuweka pesa moja kwa moja kwenye akunti yako ya Meridianbet kwa kutumia mtandao wa Airtel. Usipate wasi wasi, tunaifanya kazi kuwa rahisi zaidi!

Soma Zaidi

 

35 Komentara

    Mapambano dhidi ya Corona ni safari ndefu sana kwa ulimwengu, Mungu atufanyie wepesi

    Jibu

    Duuuuh! Hatar sana nilitarajia kumuona eliud kipchonge ndan ya marathon akifanya maajab tena ya kuchukua medal tena but corona inapoteza raha ya michuano sana

    Jibu

    Daah pole sana kwa hilo

    Jibu

    Corona ttz

    Jibu

    Duuh mbona majanga hayaishi

    Jibu

    Duu hali ishakuwa tete Mambo mengi huludi nyuma kukalishwa kwavitu vingi Sana Corona inalostisha sana

    Jibu

    Duuh hii Corona hii nie shiida

    Jibu

    Hii corona hii tuombe tu Mungu

    Jibu

    Corona tishioo kwa wenzetu

    Jibu

    Corona imeharibu kila kitu

    Jibu

    Pole Sana corona imeharibu Sana Mambo mengi hasa kwa ulimwengu wa soka

    Jibu

    Mungu aendelee kutuepusha na hili janga

    Jibu

    Daah hii corona ni changamoto sana

    Jibu

    Kinga bora kuliko tiba!!!

    Jibu

    Hii Corona sio powah kwa kweli

    Jibu

    Duuhh covid 19 imeharibu kila kitu

    Jibu

    Corona noma

    Jibu

    Corona imekosesha mambo mengi

    Jibu

    Korona himearibu mambo mengi kweli daaah..!habari mbaya kwa mashabiki wa mbio za Marathon

    Jibu

    Nakala nzuri #meridianbettz

    Jibu

    Corona bado ni janga duniani

    Jibu

    Duh majanga ya covid 19

    Jibu

    Covid imefanya michezo kukosa radha

    Jibu

    mungu awasaidie jamani na hili gonjwa

    Jibu

    corona shida

    Jibu

    Michez mingi imeahilishwa kutokan na janga hili

    Jibu

    Corona hatari

    Jibu

    Mungu awaepushie nahilo gonjwa

    Jibu

    Daah corona inafelishwaa kweli

    Jibu

    Mapambano ya corona ni safar ndefu wakati mwngn unaweza kufananisha na bahari cjui lini itakimbia duniani, ulimwengu inabid imgeukie mung kwa maomb Zaid.

    Jibu

    Mhhh corona siyo poa

    Jibu

    dah sasa hii balaa shindano tulikuwa tunalisubiri kwa hamu kubwa sana hii corona balaa tupu

    Jibu

    Duh corona inazingua

    Jibu

    Covid 19 inatisha

    Jibu

    Mh!!!corona shida

    Jibu

Acha ujumbe