Torino wamethibitisha rasmi kumsajili beki wa pembeni Valentino Lazaro kwa uhamisho wa kudumu kutoka Inter, baada ya kuutumia msimu wa 2022-23 kwa mkopo na Granata.
Inaaminika kuwa Torino imelazimika kulipa Nerazzurri ada ya €4m pamoja na kifungu cha 10% cha kuuzwa kwa Lazaro, ambaye alikuwa amebakiza mwaka mmoja kwenye kandarasi yake huko San Siro. Mchezaji huyo wa kimataifa wa Austria sasa amesaini mkataba wa miaka minne, ambao utaendelea hadi msimu wa joto wa 2027.
Odds kubwa kasino ya mtandaoni na michezo ya sloti ni vitu vinavyoweza kubadilisha maisha yako kwa kukupatia pesa nyingi. Ingia mchezoni hapa.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 aliichezea Inter mara sita pekee katika Serie A wakati wa kukaa kwake kwa miaka minne, lakini alitumia muda mwingi nje kwa mkopo akiwa na Newcastle, Borussia Moenchengladbach, Benfica na hivi majuzi akiwa Torino.
Hapo awali alikuwa ameiwakilisha Hertha Berlin kwenye Bundesliga kwa miaka miwili, baada ya kujiunga na RB Salzburg mnamo 2017.
Aviator, poker, Roullette, Wild Icy Fruits, Piggy Party na mingine kibao upige pesa na Meridianbet. Ingia www. meridianbet.co.tz.
Lazaro anatarajiwa kuchukua nafasi ya Wilfried Stephane Singo, aliyeondoka klabuni hapo na kujiunga na AS Monaco wiki iliyopita.