Klabu ya Vipers ya nchini Uganda imemtimua kocha wake Roberto Luiz Bianchi baada ya kuwa na mwendelezo mbaya wa matokeo kwenye michuano ya Klabu Bingwa Afrika.

Roberto toka michuano hii ianze hajashinda hata mechi moja hadi sasa huku akiwa ndiye kibonde wa Kundi C ambapo mechi mbili ametoka kupoteza dhidi ya Simba akiwa nyumbani kwake na ugenini.
Katika michezo minne ambayo amecheza ni mchezo mmoja tu ambao amepata pointi moja lakini yote amepoteza. Mechi ijayo ya klabu Bingwa Vipers atamenyana dhidi ya Raja Casablanca mabye ndiye kinara wa kundi hilo.
Halafu baada ya hapo atamalizana na Horoya kukamilisha ratiba yake kwenye michuano hii ya klabu bingwa.

Robrto Luiz ameiacha timu hiyo nafasi ya 4 wakiwa na pointi zao 28 baada ya kucheza michezo yao 15, wakishinda nane, sare nne, na kupoteza mara tatu.

