Kocha wa Real Madrid, Zinedine Zidane amethibitishwa kuwa na virusi vya corona.
Klabu hiyo ya Uhispania alitoa taarifa fupi iliyotangaza kwamba kocha huyo wa miaka 48 amepata maambukizi ya virusi vya corona lakini haikutoa taarifa zaidi kuhusu hali yake au ikiwa hilo litaathiri kwa namna yoyote ile kikosi chake.

Zidane anapitia shinikizo kwa matokeo mabaya ya timu hiyo ya Real ikiwemo mechi ya Jumatano katika taji la Copa del Rey waliposhindwa na timu ya Alcoyano.
Real Madrid, ikiwa ni ya pili baada ya mahasimu wao Atletico katika Ligi ya La Liga itachuana na Alaves Jumamosi .
Kupoteza mchezo dhidi ya Alcoyano kunawadia ikiwa ni wiki moja baada ya kuondolewa kwenye kombe la Super Cup na Athletic Bilbao.
Real Madrid inayoshika nafasi ya pili katika jedwali imecheza mechi 18, wakiwa alama 7 nyuma ya Atletico, ambayo ina mechi 2 ambazo haijacheza.
Pokea mualiko wa Meridianbet na Pragmatic Play kutengeneza mkwanja kwenye kasino ya mtandaoni sasa. Jiunge sasa kupata ishindi huu.



Sania
Covid sio poa
Adelta
Coronavirus sio poa mwenyezi mungu atuepushe
Rahmal
Pole sana zidane corona noma sana
Dorophina
Majanga juu ya majanga kwa zidane pole yake
Magdalena
Zidane nae majanga yanamuandama
Caroline
Pole Sana Zidane
Lydia Emmanuel Magoti
Daah pole yake zidane
Hopemwaikuka
Ugua pole Z
Sarah
Zidane mungu akusimamie upone
Ernest Kimeru
Hatari hii
Issa
Covid ni balaa
warda
Jamani pole yake