Mshambuliaji wa zamani wa Chelsea na Manchester United Romelu Lukaku alizungumzia kuhusu jeraha lake baya la hivi karibuni pamoja na yale ya nyuma hali yaliyomfanya kuwa nje ya uwanja kwa muda mrefu akijiuguza.

Kupitia mahojiano maalum aliyoyafanya na Skysport Italia Lukaku alieleza mambo mengi sana ikiwemo jeraha lake la hivi karibuni alilopata na kumfanya akae nje kwa muda mrefu.
“Ilikuwa ni jeraha kubwa sana. Kwa kawaida mimi hupona haraka kutokana na majeraha, lakini wakati huu nilikuwa na hisia kwamba mambo hayaendi sawa. Ilikuwa mara ya kwanza katika miaka 13 kwamba nilikosa michezo mingi. Ukija nyumbani kwangu inaonekana kama hospitali….
“Nina kila kitu cha kupona haraka niwezavyo, lakini wakati huu sikuweza. Nilikwenda Kombe la Dunia na kucheza mchezo wa mwisho, nilikuwa na vipindi viwili tu kwenye miguu yangu katika miezi minne iliyopita.
“Dhidi ya Croatia ilikuwa tamaa kubwa, lakini nilijiambia, Lukaku, haukuwa fiti kwa 100%, ulikuwa umefanya mazoezi mara mbili….
“Sasa ondoka, pumzika siku tano na tunaanza kutoka mwanzo. Nilienda Dubai na mkufunzi wa timu ya taifa na sasa niko tayari. Waliondoa kwa haki lakini sasa nina hamu sana ya kurudi uwanjani tena. Kuanzia sasa tuzungumze uwanjani!”
Lukaku pia aligusia hali ya timu ya taifa ya Ubelgiji na hatua zinazofuata kwa nchi yake huku akimwaga sifa nyingi kwa Thiery Henry akitamani awe kocha mkuu.

“Kwangu mimi, Henry atakuwa kocha ajaye wa Ubelgiji. Hakuna shaka juu yake. Nitasema wazi, atakuwa kocha anayefuata. Ana heshima ya wachezaji wote, ameshinda kila kitu. Anajua kufundisha, anajua tunachopaswa kufanya ili kufika hapo. Anajua timu, ligi na wafanyikazi.
“Kwangu mimi ndiye kocha bora kwa timu yetu ya taifa. Halafu sijui watampata nani. Lakini sidhani kama Ubelgiji inapaswa kuanza kutoka mwanzo. Kufikia sasa, kizazi hiki hakijashinda, lakini lazima tuendelee kujaribu kushinda.
“Anataka kushinda, na sidhani kama shirikisho linakwenda na kupata kocha ambaye anataka kubadilisha kila kitu na kuanza kutoka mwanzo. Kwangu mimi, haifai.”

