Inonga Azidi Kuimarika Huko Mazoezini

Beki wa kati wa Simba Henock Inonga Baka ‘Varane’ ameonekana akizidi kuimarika kwenye viwanja vya mazoezi Bunju jijini Dar es Salaam.

 

Inonga Azidi Kuimarika Huko Mazoezini

Beki huyo kwa muda mrefu alikuwa majeruhi na amekosekana kwenye michezo kadhaa ya Simba akiwa sambamba na baadhi ya mastaa wengine kama kiungo Mmalawi, Peter Banda na mshambuliaji Mzambia Moses Phiri.

Meneja wa Kitengo cha Mawasiliano na Habari, Ahmed Ally amewaambia wanamsimbazi kuwa ”Sasa Inonga amepona.”

Inonga Azidi Kuimarika Huko Mazoezini

Beki huyo aliumia toka mechi ambayo Simba walikuwa Kagera Kaitaba kukiwasha dhidi ya Kagera Sugar kwenye mchjezo ambao ulimalizika kwa Msimbazi kulazimishwa sare ya kufungana bao 1-1 dhidi ya Wanankurukumbi.

Simba inatarajia kushuka kesho dimbani dhidi ya Singida Big Stars ambapo mechi ya kwanza kumenyana walitoshana nguvu.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.