Beki wa klabu ya Simba Henock Inonga ambaye alipata majeraha katika mchezo wa ligi kuu ya NBC dhidi ya klabu ya Mbeya City na kumfanya kukaa nje ya uwanja kwa kipindi fulani sasa amerejea mazoezini rasmi.
Beki huyo amerudisha matumaini kwa mashabiki wa Simba kutokana na kurejea kwa beki huyo kutokana na umuhimu wake ndani ya kikosi cha Simba. Inonga ameanza mazoezi na wenzake ndani ya kikosi cha Simba kwa mara ya kwanza leo.
Henock Inonga amekaa nje ya timu kwa takribani wiki mbili sasa baada ya kupata majeraha katika mchezo dhidi ya Mbeya City, Taarifa za awali zilieleza kua huenda beki huyo angekaa nje ya uwanja kwa muda mrefu lakini imekua tofauti kidogo kwani ameweza kurejea ndani ya muda mfupi.
Kurejea kwa beki huyo sasa kunaiweka klabu ya Simba kwenye mikono salama katika safu ya ulinzi ya klabu hiyo, Safu ya ulinzi ya klabu ya Simba ilionekana kutetereka katika michezo miwili iliyocheza bila ya kua na beki huyo mwenye ubora mkubwa.
Beki Henock Inonga baada ya kurejea mazoezini rasmi ndani ya klabu ya Simba sasa anatarajiwa kuwepo katika michezo ya ligi kuu ya NBC pamoja na michuano mingine, Klabu ya Simba inajiandaa na michuano mbalimbali ikiwemo NBC, FA, na ligi ya mabingwa Afrika hivo wanahitaji kua na wachezaji wao muhimu na beki huyo ni miongoni mwao.

