Mikel Arteta Anasisitiza Kwamba Kuna 'mengi zaidi' Kutoka kwa Gabriel Martinelli

Kocha wa Arsenal Mikel Arteta anaamini kwamba kuna ‘mengi zaidi’ yanakuja kutoka kwa Gabriel Martinelli, baada ya Mbrazil huyo kusaini mkataba mpya wa miaka minne na nusu na Washika Mtutu. Odds kubwa za soka unazipata Meridianbet.

 

Gabriel Martinelli

Klabu hiyo ilithibitisha habari hizo kwenye mitandao ya kijamii Ijumaa asubuhi, huku kandarasi hiyo ikimbakiza winga huyo wa Brazil kwenye viunga vya Emirates hadi msimu wa joto wa 2027. Arsenal pia wana chaguo la kuongeza miezi 12 zaidi.

Mkataba wake wa awali ulitarajiwa kumalizika mwishoni mwa msimu ujao, ingawa klabu hiyo ilikuwa na chaguo la kuongeza mkataba huo kwa miaka miwili zaidi.

Arteta aliiambia tovuti rasmi ya klabu: “Tuna furaha kwamba Gabriel Martinelli amesaini mkataba mpya wa muda mrefu.

 

arteta

“Wafuasi wetu wanaona ubora na nguvu zake kila mara anapovaa shati na yuko sawa kila siku katika mazoezi, kwa bidii yake na maadili mazuri.

“Gabriel Martinelli bado ni mdogo sana, kwa hivyo tunajua bado kuna mengi zaidi kutoka kwake na ni vyema tutakuwa katika safari hii pamoja. Sasa tunafuraha kuendelea kukuza kipaji chake kikubwa na tunatazamia kumuona akicheza na Arsenal katika miaka ijayo.’

Gabriel Martinelli, katika video iliyochapishwa na klabu hiyo kwenye mitandao yao ya kijamii, alisema kwamba Arsenal ni ‘klabu yake’ na kwamba anapenda kila kitu kuhusu The Gunners. Beti na Meridianbet mechi za ligi zote, odds ni kubwa sana, Usikose hii!!.

Aliongeza: “Nilizaliwa mbali sana kutoka kaskazini mwa London lakini mara tu nilipofika hapa wafuasi wetu walinifanya nijisikie kama mmoja wao.

“Haikunichukua muda mrefu kutambua kwamba mahali hapa palikuwa zaidi ya soka. Ni kuhusu sisi, urithi wetu, umoja wetu na jamii yetu ambayo unapaswa kuelewa.

“Siku baada ya siku tunapata uzoefu tunatengeneza kumbukumbu mpya pamoja na kuhisi fahari. Najisikia nikitembea barabarani mtu anaposema “wewe ulikuwa mwenzangu”. Kwa hivyo asante Arsenal kwa kunifanya nijisikie nyumbani.”

Mkurugenzi wa michezo Edu alipigwa picha akiwa na Arteta na Gabriel Martinelli, huku wa mwisho akisaini mkataba wake mpya. Ukiwa na meridianbet unaweza kubashiri mubashara, tembelea maduka ya meridianbet uweze kubashiri.

Edu alisema: “Ni vizuri kwamba Gabriel Martinelli amesaini mkataba mpya nasi. Misingi ya kikosi chetu inaendelea kujengwa katika vipaji vya vijana, hivyo ni vyema Gabi amesaini mkataba mpya.

“Gabi bado ana umri wa miaka 21, na ni mchezaji mwenye uwezo mkubwa na haiba. Yeye ni sehemu muhimu ya mustakabali wetu na tunafurahi kwamba tumekubali mkataba mpya.”

Mkataba mpya wa Martinelli unakuja wakati mzuri kwa Mbrazil huyo huku ushindani mzuri ukionekana kuongezeka Emirates. Meridianbet wanatoa ODDS kubwa kwenye mechi zote. Bashiri hapa.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.