Klabu ya Manchester United rasmi wamepeleka kiasi cha Euro milioni 60 kwa klabu ya Atalanta kwajili ya mshambuliaji wa klabu hiyo Rasmus Hojlund.
Manchester United inafahamika kwasasa kipaumbele chao cha kwanza ni kupata mshambuliaji mwenye uwezo wa kuimarisha safu ya ushmabuliaji ya klabu hiyo na Rasmus Hojlund ndio amekua chaguo lao la kwanza kwasasa.
Klabu hiyo imetuma ofa ya Euro milioni 60 ambayo 50 italipwa kwasasa halafu 10 iliyobakia watalipa kutokana na vipengele ambavyo watakubaliana na klabu ya Atalanta kwajili ya mshambuliaji huyo ambao wapo vitani na klabu ya PSG.
Man United wanatambua kua klabu ya PSG pia inamtaka Rasmus Hojlund kuelekea msimu ujao na ndio sababu wanahitaji kumalizana na Atalanta mapema, Lakini masgetani hao wekundu wameshamalizana na mchezaji huyo kwenye maslahi yake wiki kadhaa nyuma.
Klabu ya Atalanta wanaelezwa kusimamia msiamamo wao wa kuhitaji kiasi cha Euro milioni 70 kama ambavyo walibainisha hapo awali, Hii inaonesha wazi kua Manchester United watahitajika kuongeza kiasi cha Euro milioni 10 katika ofa yao ya awali waliyoipeleka.

