GAMONDI AFUNGUKA UJANJA WA YANGA YAKE

Kocha Mkuu wa Yanga Muargentina Miguel Gamondi amezipa tahadhari timu za Ligi Kuu Bara. Hiyo ni baada ya timu yake kuanza vema kwa kushinda mechi mbili mfululizo mabao 5-0 walipocheza dhidi ya KMC na JKT Tanzania.

 

GAMONDI AFUNGUKA UJANJA WA YANGA YAKE

Yanga pia ilipata ushindi wa mabao 5-1 walipocheza dhidi ya ASAS FC ya nchini Djibouti katika Ligi ya Mabingwa Afrika.

Gamondi alisema kuwa timu pinzani hazitakiwi kujilinda zaidi wanapokutana na badala yake kufunguka kwa kucheza soka kama hawataki kufungwa tano.

Gamondi alisema kuwa timu yake inapata ugumu inaopokutana na wapinzani wanaocheza soka la pasi na kushambulia, hiyo inawafanya wapate ugumu wa kushambulia.

GAMONDI AFUNGUKA UJANJA WA YANGA YAKE

Aliongeza kuwa timu ikijilinda sana, inawapa nafasi ya wao kufanya mashambulizi kwa kasi huku wakianza kuwakabia kuanzia golini kwa wapinzani.

“Wapinzani wenyewe ndio wanataka tuwafunge mabao matano, ni kutokana na kucheza soka la kujilinda kwa kukaa wengi golini kwao. Wao kama hawazitaki tano, basi wasijilinde na badala yake wanapaswa kushambulia kwa kucheza soka la pasi.”

Kwani wakijilinda sisi tunapata nafasi ya kushambulia goli la wapinzani kwa kasi tukiwatumia viungo kupiga pasi za mabao, alisema Gamondi.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.