Mchezaji wa zamani wa akademi ya Bayern Munich na gwiji wa timu ya taifa ya Ujerumani Toni Kroos hajawahi kuwa mtu wa kuficha maneno yake.

Katika toleo la hivi karibuni la podikasti yake Einfach mal Luppen, Kroos alieleza wasiwasi wake kuhusu matatizo ya Bayern Munich katika kulinda mipira ya adhabu ya kudumu (set pieces).
“SioniAtalanta BC kama kikwazo kikubwa kwa sasa. Lakini unapofika kwenye mechi dhidi ya Manchester City au Real Madrid baadaye… ni kweli kwamba siku hizi mechi nyingi zinaamuliwa kupitia mipira ya adhabu ya kudumu,” alisema Kroos.
Kroos alisema kuwa anaamini hata kama si rahisi kuzuia mipira hiyo, idadi ya mabao wanayofungwa kupitia hali hiyo ni kubwa sana na inaweza kumaliza haraka msimu ambao kwa ujumla unaenda vizuri.
Meridianbet inakwambia kuwa endelea kubashiri hapa kwani ODDS KUBWA na machaguo zaidi ya 1000 yapo hapa. Ingia kwenye akaunti yako na uanze safari yako ya ushindi sasa.


