Kocha wa klabu ya Manchester City, Pep Guardiola, amesema timu yake italazimika kushinda mechi zote zilizobaki ili kufanikiwa kutwaa ubingwa wa Premier League, baada ya kupanda kileleni mwa msimamo wa ligi kwa ushindi mwembamba dhidi ya Burnley.
Manchester City walishinda 1-0 dhidi ya Burnley, matokeo yaliyowaweka kileleni mwa ligi kwa mara ya kwanza tangu mwezi Agosti na kuifanya mbio za ubingwa kuwa kali zaidi kati yao na wapinzani wao wakubwa.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Guardiola alisema “Tulicheza vizuri sana, lakini tulikosa nafasi nyingi za kufunga. Tuliboresha ulinzi katika kipindi cha pili na tulikuwa na udhibiti zaidi wa mchezo.”
Akizungumzia changamoto ya ratiba ngumu, aliongeza “Tulicheza mchezo mgumu sana Jumapili, na baada ya siku tatu si rahisi. Lakini kwenye Premier League lazima ujipange haraka na sisi tumezoea hilo.”
Kocha huyo pia alikiri kuwa ushindi mwembamba unaongeza presha katika mbio za ubingwa akisema “Sasa tuna mechi ya FA Cup kisha tunabaki na mechi tano. Njia pekee ni kushinda kila mchezo.”
Guardiola alisisitiza kuwa makosa ya kupoteza nafasi za wazi yanaweza kuwagharimu kwenye mbio hizo, akihimiza wachezaji wake kuwa makini zaidi katika michezo ijayo ya mwisho wa msimu.
Kwa ushindi huo, Manchester City sasa wanaendelea kuongoza ligi, huku mbio za ubingwa zikitarajiwa kuwa kali hadi mchezo wa mwisho wa msimu.

