Barcelona wamekubali kumwachilia mshambuliaji Luis Suarez ajiunge na washindani wakuu katika Ligi Kuu ya Uhispania (La Liga), Atletico Madrid.
Suarez hatakikani kabisa kambini mwa Barcelona ambao kwa sasa wanatiwa makali na kocha mpya Ronald Koeman.
Miamba hao wa soka ya Uhispania walikuwa radhi kumwachilia Suarez ambaye ni raia wa Uruguay kujiunga na kikosi chochote bila ada ilmradi klabu ambayo angejiunga nayo si ya La Liga.

Suarez alihiari kupunguziwa mshahara ili kuingia katika sajili rasmi ya Atletico baada ya uhamisho wake hadi Juventus ya Italia kugongwa mwamba kwa sababu ya changamoto za kutafuta pasipoti na kibali cha kufanyia kazi Italia.
Rais wa Barcelona, Josep Maria Bartomeu alizuia uhamisho wa Suarez hadi Atletico kwa sababu hakutaka nyota huyo auzwe kwa kikosi ambacho ni washindani wao wakuu ligini.
Hata hivyo, baada ya kukutana na wawakilishi wa Suarez, vinara wa Barcelona waliafikiana nao baada ya fowadi huyo wa zamani wa Liverpool kufichua mipango ya kuanika kwenye vyombo vya habari jinsi “anavyohangaishwa” na Barcelona.
Atletico kwa sasa wameweka mezani kima cha Sh448 milioni kwa minajili ya huduma za Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 33.

Hata hivyo, fedha hizo huenda zikaongezeka kutegemea jinsi atakavyowajibishwa na Atletico na iwapo ataongoza kikosi hicho cha kocha Diego Simeone kupiga hatua zaidi kwenye soka ya Klabu Bingwa Ulaya (UEFA).
Uhamisho wa Suarez unatamatisha kipindi cha miaka sita ya usogora wake kambini mwa Barcelona ambao amewafungia jumla ya mabao 198 kutokana na mechi 283.
Katika enzi za ubora wake, Suarez alishirikiana vilivyo na Lionel Messi na Neymar muungano wao almaarufu MSN ukawa tishio zaidi kwa mabeki wa kikosi chochote duniani.
Mshambuliaji huyo alijiunga na Barcelona mnamo 2014 baada ya kuagana na Liverpool kwa kima cha Sh10.3 bilioni. Tangu wakati huo, ameshindia Barcelona mataji manne ya La Liga, manne ya Copa del Rey, moja la UEFA na jingine la Kombe la Dunia mnamo 2015.
FURAHIA KASINO YA MTANDAONI
Tembelea ardhi ya maajabu ushangazwe na mengi ikiwa ni pamoja na urahisi wa kujipatia utajiri kupitia Kasino ya Meridianbet.


Ester jackson
Kila la heri Suarez Barcelona wabinafsi sana wameona wakuachie huko ambako hakuna upizani mana wanajua moto wako
magdalena
piga kazi suarez nakuaminia unaga kazi mbovu ukiwa uwanjani
Mwajumah
Kila la kheri suarez
Dorophina
Kapige kazi suarez Madrid wamekuamini
Shan
Kipenda roho ula nyama mbichi
Elika
Safi sana kama Suarez akienda huko
Fatina
Itakuwa powah snaa kma hataenda kubadilisha upepo!!
Adelta
Vizuri Sana suarez kapige kazi
Sauda
Piga kaz kijana.
Ernest
Kweli ni wakati mgumu na maamuzi magumu sana kwa Barca, Kila la heri Suarez
Caroline
Barcelona kazi wanayo mbona…
Angelina
Kila kheri
Lydia Emmanuel Magoti
Suarez Mambo ya shajipa
Nasra
Suarez kila la kheri
Rehema
Kila la kheri
aisha
Kapige kazi broo suarez kila la kher huko uendako
Janeflora malisa
Asnt kwa taarif
Venerose
Kazi popote
Tatu
Kila la khery suarez
Samira
Bora tu suarez alivyopata nafasi huko atletico
farida ahmadi
Kila la kheri Suarez
Rehema Dickson
Kapige kazi suarez Madrid wamekuamini
Saupha mohamed
Safi piga Moira mzeee
Neema
Kila la kheri
Fatuma kasomo
Safi sana
Tahiya
Hatimaye katua hapo
Johnmary joel
Hongera zake#meridianbett
Amiri Kayera
Pale A.madrid atafunga sana
Theonestina
Kila la kheri
Sabrina
Sio mbaya
Tumaini kasalile
Safi sana
Aziza mushi
Kila la kheri
Gabriel
Safi sana 👍
Samiah
Safi sanaaa
Zeiyana
Si zani kama Suarez hatabaki atletico kwa miaka yake yote hatakua kwa mda tu ili kutimiza malengo yake yakutoka Barcelona
Rose kapinga
Suarez yuko vizuri!!
Hopemwaikuka
All ze best
Issa
Safi pia kubadii upepo
David Pere
Uhamisho wa Suarez unatamatisha kipindi cha miaka sita ya usogora wake kambini mwa Barcelona ambao amewafungia jumla ya mabao 198 kutokana na mechi 283.