Ofisa Mtendaji Mkuu wa Simba SC, Barbara Gonzalez amefunguka kuwa wamekuja kushinda mechi hiyo, dakika chache baada ya timu hiyo kuwasili mkoani Kigoma kwa maandalizi ya mchezo wa fainali ya kombe la Azam (ASFC) dhidi ya watani zao Yanga.
“Tumefika Kigoma salama na kilichotuleta ni kutafuta ushindi tu. Wachezaji wetu wako vizuri na wanalitambua hilo, tumeona namna Mashabiki wetu walivyotupokea kwa wingi wakiwa na furaha hivyo tutapambana kushinda ili kuwaheshimisha,” amesema Barbara.
Simba SC wana kumbukumbu ya kupoteza mchezo wa ligi kuu dhidi ya Yanga kwa goli 1-0 katika mchezo uliopigwa katika dimba la Mkaba jijini Dar es salaam wiki mbili zilizopita.
Simba SC ambao ni mapingwa wapya wa Ligi kuu ya Tanzania bara msimu huu wanataka kutwaa kombe hilo la Azam ASFC ili kulipiza kisasi kwa watani wao kutokana na mchezo uliopita.
Kasino ya Mayan Eagle inakukufanya kuwa bingwa wakati wowote unapoamua kuicheza. Utaburudika huku ukiendelea kutengeza mkwanja mrefu, jiunge sasa na uwe miongoni mwa mabingwa!!



Ernest
Ukiangalia Simba wanaonekana kuwa na kikosi kipana hivyo kuwapa Asilimia kubwa sana ya kushinda katika hii mechi, Lakini kitamaduni mechi ya Simba na Yanga ni Zaidi ya Mpira uwanjani, Ngoja tuone.