Kocha wa zamani wa Warriors, Zdravko Logarusic anatajwa kuongoza mbio za kuchukua mikoba ya kukinoa kikosi cha Simba SC iliyoachwa na Didier Gomes Da Rosa.

Logarusic alifungashiwa virago mwezi uliopita baada ya kuanza vibaya akishinda mechi moja kati ya kumi na nne alizosimamia kikosi hicho.
Kulingana na taarifa mbalimbali zinaeleza kocha huyo yupo tayari kuchukua mikoba ya Da Rosa ambaye aliachana na timu hiyo siku chache baada ya Simba SC kuondolewa katika Ligi ya Mabingwa Barani afrika dhidi ya Jwaneg Galaxy.
Ikumbukwe, Loga alishawahi kukinoa kikosi cha Simba SC katika msimu wa 2013 na 2014.
Mchongo wa mkwanja mrefu kutoka kasino bora za mtandaoni za Meridianbet. Mchezo wa Circus Fever unakuweka katika nafasi nzuri ya kuwa mshindi. Furahia kasino maridhawa kutoka nyumba ya mabingwa meridianbettz.

CHEZA HAPA

