Mapema mwanzoni mwa msimu ilikuwa ni Mikel Arteta mbaye alikuwa anakumbana na presha ya kupoteza kibarua chake kwenye timu ya Arsenal sasa mambo yamebadilika ni Ole Gunnar Solskjaer sasa ndiye mwenye presha ya kupoteza kibaru chake.
Nafasi ya Solskjaer kwenye klabu ya mashetani wekundu imakalia kuti kavu baada ya wikiendi iliyopita kupokea kichapo kitakatifu cha goli 5-0 kutoka kwa mahasimu wao Liverpool, huku tetesi za kupoteza kazi zimekuwa zikiongezeka pia kukiwa na tetesi za kutafutwa mrithi wake kwenye viunga vya Carrington Park.

Mikel Arteta kwenye kikao na waandishi wa habari alipoulizwa kuhusu Solskjaer kuhusu na matokeo mabaya ya hivi karibuni alisema, “mara zote ni kuhusu matokeo, wote tunajua mambo mengine yote hyajarishi sana.”
“Unapokuwa na matokeo mabovu ni sawa kwa kila mtu, sio kipindi kizuri kwa yeyote anayepitia hilo, najua anapitia kipindi kigumu.”
Man Utd haijashina kwenye michezo yake minne ya mwisho kwenye ligi kuu mpaka sasa, na Solskjaer anaamini ushindi dhidi ya Tottenham kesho ndio utampa mwangaza mpya kuhusu kutetea kibarua chake
Mchongo wa mkwanja mrefu kutoka kasino bora za mtandaoni za Meridianbet. Mchezo wa Circus Fever unakuweka katika nafasi nzuri ya kuwa mshindi. Furahia kasino maridhawa kutoka nyumba ya mabingwa meridianbettz.

CHEZA HAPA

