Klabu ya Yanga SC imemtambulisha rasmi winga Denis Nkane kuwa mchezaji wa klabu hiyo. Nkane mwenye umri wa miaka 19 amejiunga kwa mkataba wa miaka mitatu akitokea klabu ya Biashara United ya Mara.

Nkane anacheza nafasi ya kiungo mshambuliaji alitambulishwa jana Jumamosi Tarehe 1 January 2022 katika kurasa za kijamii za klabu ya Yanga SC baada ya kuonyesha kiwango kikubwa akiwa na Biashara United.
Huu unakua ni usajili wa tatu kwa klabu hiyo baada ya kipa Abdultwalib Mshery kutoka Mtibwa Sugar na kiungo Salum Abubakari ‘Sure Boy’ kutoka Azam FC.
Yanga SC inashika nafasi ya kwanza katika Ligi kuu ya NBC wakiwa na alama 29 baada ya michezo 11 nyuma ya watani wao Simba SC wanaokamata nafasi ya pili wakiwa na alama 24 wakiwa pungufu ya mchezo mmoja.
Unaanzaje siku yako katika msimu huu wa sikukuu, mchongo upo meridianbet kasino. Sloti pendwa ya Sahara Richies inaweza kukufanya ukawa milionea katika kufunga mwaka huu, Jiunge na ufurahie kasino maridhawa kutoka nyumba ya mabingwa.

CHEZA HAPA

