Uongozi wa klabu ya Singida Black Stars umetangaza rasmi kufanya mabadiliko katika benchi la ufundi kwa lengo la kuimarisha utendaji wa timu hiyo katika mashindano mbalimbali.
Kupitia taarifa yao, klabu hiyo imethibitisha kufikia makubaliano ya kumuajiri Papy Kimoto kuwa Meneja Mkuu wa Timu, pamoja na Kapiten Ngoyi Dora ambaye atahudumu kama Kocha Msaidizi, wote wakisaini mikataba ya mwaka mmoja na miezi mitatu.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Wakati huo huo, Muhibu Kanu ataendelea kubaki kwenye nafasi ya Kocha Mkuu hadi mwisho wa msimu huu, akitarajiwa kuongoza majukumu yote ya kiufundi kwa kushirikiana na benchi jipya la ufundi.
Kwa mujibu wa uongozi wa klabu hiyo, mabadiliko hayo yanalenga kuleta ufanisi zaidi ndani ya kikosi, kuimarisha nidhamu ya wachezaji pamoja na kuongeza ushindani unaohitajika katika ligi.
“Uongozi una imani kuwa muundo huu mpya utaimarisha utendaji wa timu, kuongeza nidhamu na kurejesha ushindani unaotarajiwa,” imeeleza sehemu ya taarifa hiyo.

