Geita Gold Kutimua Vumbi Dhidi ya Polisi Tanzania Kesho

Ligi kuu ya NBC inatarajiwa kuendelea hapo kesho kwa michezo miwili, ambapo mchezo wa mapema kabisa utakuwa kati ya Geita Gold dhidi ya Polisi Tanzania majira ya saa 10:00 jioni.

 

Geita Gold Kutimua Vumbi Dhidi ya Polisi Tanzania Kesho

Mchezo huo utapigwa katika uwanja wa Nyankumbu huku timu zote zikitafuta pointi 3 ili kujiweka kwenye nafasi nzuri ya msimamo kwenye ligi kuu.

Geita wapo nafasi ya 5 baada ya kucheza michezo 20, wakiwa wameshinda mechi zao sita, sare tano na kupoteza michezo mitano, wakijikusanyia pointi zao 27 hadi sasa kwenye Ligi.

Geita Gold Kutimua Vumbi Dhidi ya Polisi Tanzania Kesho

Wakati kwa upande wa Polisi Tanzania wapo nafasi ya mwisho kwenye msimamo baada ya kuvuna pointi zao 14 kwenye michezo 20 waliyocheza, wakiambulia ushindi mara 3, sare 5 na vipigo 12.

Mechi zilizopita za timu hizo mbili wote walishinda, lakini mechi tatu za mwisho kukutana kati yao Wachimba Madini wameshinda zote. Kesho Polisi atakubali kichapo tena?

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.