Kocha mkuu wa Yanga Nasreddine Nabi ametwaa tuzo ya kocha bora wa mwezi Oktoba baada ya kuwa na mfululizo mzuri wa matokeo latika Ligi kuu ya NBC huku akiwa hajapoteza mchezo wowote msimu huu toka uanze.
Nabi na timu yake mwezi Oktoba wamecheza mechi nne, ambapo tarehe 3 Oktoba walicheza dhidi ya Ruvu Shooting wakashinda 2-1, mechi inayofuata ya pili walikipiga dhidi ya Simba katika Dabi ya Kariakoo na kutoa sare ya 1-1.
Mechi ya tatu ya mwezi Oktoba walicheza tarehe 26 dhidi ya KMC na kushinda kwa bao 1-0 na mechi ya mwisho wakaja wakacheza dhidi ya Geita Gold CCM Kirumba na wakashinda bao 1-0 pia.
Klabu hiyo inatarajia kuingia Dimbani leo kukipiga dhidi ya Kagera Sugar ya Mecky Mexime kuzitafuta pointi 3 muhimu ambazo akizipata khuenda akarudi katika nafasi yake ya kwanza ambayo kwasasa yupo Azam fc.
Nabi na vijana wake wana michezo miwili mikononi na inabidi washinde vyote kama wanataka kutetea taji lao ambalo walilipata msimu uliopita huku kocha akilalama kuhusu ratiba ambayo wako nayo.
Ulishawahi kuwaza kuwa rubani wa maisha yako!! Kuwa rubani wa mchezo pendwa wa Aviator wa kasino mtandaoni. Aviator bonanza inazidi kutoa michongo ya mkwanja kwenye nyumba ya mabingwa. Unarusha ndege yako na unashinda, kuwa rubani wa kujivunia kwa kuibuka na mkwanja leo.
BONYEZA HAPA