Pazia la Ligi Kuu Kufunguliwa Leo ni Pamba Jiji vs Tz Prisons

Hatimaye pazia la ligi kuu ya NBC Tanzania linaenda kuzinduliwa hii leo kwa mchezo mmoja ambapo wenyeji Pamba Jiji ambao wamepanda daraja msimu huu watakiwasha dhidi ya Tanzania Prisons.

Pazia la Ligi Kuu Kufunguliwa Leo ni Pamba Jiji vs Tz Prisons

Mchezo huo utapigwa majira ya saa 10:00 jioni ambapo Prisons msimu uliopita, alishika nafasi ya 9 kati ya timu 16 huku timu hiyo kutoka jijini Mbeya ikiwafunga Wekundu wa Msimbazi msimu uliopita.

Pia meridianbet inatoa michezo ya kasino ya mtandaoni kama vile, Aviator, poker, Roullette, sloti na mingine kibao. Ingia meridianbet na ucheze sasa.

Pamba Jiji wao baada ya miaka 23 iliyopita kushuka daraja na sasa wapo ligi kuu kupambania taji, huku timu hiyo ikiwa chini ya Goran Kopuvonic wanaanza kibarua chao dhidi ya Wajelajela ambao wanapewa nafasi kubwa kushinda leo.

Pazia la Ligi Kuu Kufunguliwa Leo ni Pamba Jiji vs Tz Prisons

Timu hiyo ambayo ina makazi yake Jijini Mwanza walishuka daraja 2001 hivyo sasa leo hii wanaanza kusakata kabumbu wakihitaji pointi tatu za ushindi.

Je nani ataanza ligi kwa ushindi leo au timu hizi mbili zitagawana pointi?.

Acha ujumbe