Vyanzo vya Habari nchini Misri vinaripoti kwamba Mabingwa wa Afrika, Al Ahly wako kwenye mpango wa kumsajili winga wa klabu ya Simba, Luis Miquissone mwenye umri wa miaka 25.
Luis Miquissone yupo kwenye mipango ya klabu hiyo endapo watashindwa kufikia makubaliano kwenye usajili wa Soufiane Rahimi wa Raja Casablanca na Gaston Sirino wa Mamelodi Sundowns.
Inasemekana pia klabu ya Simba na Al Ahly wamefikia makubaliano ya mdomo (Verbal agreement) na klabu ya Al Ahly juu ya bei ya mchezaji huyo nyota kwenye kikosi cha Simba SC.
Nafasi ya Luis Miquissone kwenye kikosi cha klabu ya Simba inatarajiwa kuchukuliwa na Emmanuel Okwi ambaye anahusishwa kurejea Msimbazi.
Kasino ya Mayan Eagle inakukufanya kuwa bingwa wakati wowote unapoamua kuicheza. Utaburudika huku ukiendelea kutengeza mkwanja mrefu, jiunge sasa na uwe miongoni mwa mabingwa!!
Ernest
Simba huenda wakapiga Pesa nzuri kwenye deal hili la Luis Miquissone kama ni kweli Al Ahly Wamtaka