Nahodha na beki wa Barcelona, Gerard Pique alitolewa nje baada ya kupata majeraha katika kipindi cha kwanza katika mechi ya La Liga dhidi ya Athletic Club.

Pique alitua chini vibaya baada ya kuruka hewani kuwania mpira dhidi ya Alex Berenguer na kupelekea kupata maumivu katika nyama za paja na nafasi yake kuchukuliwa na Ronald, 22.
Kocha wa Barcelona, Ronald Koeman alisema katika mkutano wake na waandishi wa habari kabla ya mechi kwamba mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 34 alikuwa akisumbuliwa na maumivu kiasi lakini alifanya mazoezi kama kawaida wiki hii.
Hii ni mara ya sita kwa Pique kutolewa katika mechi 13 za mwisho za La Liga, ambayo ni idadi sawa ya nyakati ambazo alibadilishwa katika mechi zake 111 za mwanzo za XI.
Baada ya mchezo huo, Barcelona ilithibitisha kwamba Pique alikuwa na shida ya nyama za paja na atapimwa ili kujua ukubwa wa jeraha hilo.
Ni muda wa kuwa milionea na kasino za mtandaoni za meridianbet, mchezo wa Sahara Riches unakupa nafasi ya kushinda mkwanja mrefu. Matajiri wa jangwani wanataka wakupe mkwanja leo.



[email protected]
DU pole yake
Sarah
Pole yao