Bayern vs Dortmund Ndani ya DFL Super Cup.


Miamba ya kandanda ya Ujerumani Bayern Munich na Borussia Dortmund ziliangukia pua mwishoni mwa wiki katika mechi zao za ligi kuu Bundesliga lakini wana fursa ya kurejea tena haraka kwenye mkondo wa ushindi.

Itakutana kwa mara ya kwanza msimu huu siku ya Jumatano dimbani Allianz Arena katika fainali ya DFL Super Cup. Washindi wa mataji mawili makuu ya nyumbani Bayern watawaalika Dortmund ambao ni makamu bingwa wa Bundesliga, kujaribu kubeba taji lao la tano katika mwaka wa 2020.

 

Bayern vs Dortmund Ndani ya DFL Super Cup.

Baada ya mechi 32 za ushindani bila kushindwa, ukiwemo ushindi wa mechi 23 za mwisho, Bayern walionja kichapo kizito cha 4 – 1 mikononi mwa Hoffenheim.

Walicheza saa 48 tu baada ya kurejea kutoka Budapest, ambako walibeba taji lao la nne katika mwaka mmoja la UEFA Super Cup dhidi ya Sevilla, ushindi uliopatikana katika muda wa nyogeza.

Kocha wa Bayern Munich Hansi Flick amekataa kutoa sababu ya uchovu wala kuwalaumu wachezaji wake kwa kipigo hicho maoni ambayo yanaungwa mkono na Thomas Müller.

 

Bayern vs Dortmund Ndani ya DFL Super Cup.

Ni wazi kuwa ingefika siku ambayo unapoteza mechi nyingine. Nadhani tulikuwa pia na nafasi moja au mbili ambazo tungeweza kurekebisha. Lakini kwa dakika 90 hatukustahili kutoka sare au hata kushinda mchezo. Hoffenheim ilifanya kazi nzuri leo. Kwa mukhtasari, tulistahili kushindwa na tutarudi Jumatano.

Macho yote yataelekezwa katika Mchezo huo unatarajiwa kuwa wa mvutano, pamoja na kuwakosa wachezaji wawili wakariba ya juu, Jadon Sancho na Thiago Alcantara aliyejiunga na Liverpool.


Beti kwa Kitochi Kushinda 300,000,000!

Unajua kuwa unaweza kushinda milioni mia tatu kwa buku tu? Ndiyo! Unaweza kushinda kwa kupiga *149*10# na kubashiri. Ingia mchezoni!

Soma Zaidi

34 Komentara

    Dortimund kama kawaida yao lazima kichapo kitembee kwa munich

    Jibu

    apo kazi ipo sizani kama bayern munich atakubali kupokea kichapo nyumbani kwake

    Jibu

    Mmh hii mechi itakua ya kukata na shoka maana Kila mtu anataka kutetea upande wake

    Jibu

    Leo kazi ipo tusubiri tuone matokeo

    Jibu

    Bayern lazima achukue ubingwa.

    Jibu

    Dortmund nawakubali

    Jibu

    Dortmund wajiandae kile kichapo walichopigwa nne Bayern asila zote watamalizia kwao kama wasipo jipanga wanaweza kupata haibu ya mwaka leo

    Jibu

    Dortmund lazima akiwashe

    Jibu

    Wote wapo vinzur itakuwa big game

    Jibu

    Mbona wameanza vibaya

    Jibu

    Daah hii mechi ya kukata na shoka maana timu zote zipo mstari wa mbele.

    Jibu

    Dk 90 zitatoa majibu

    Jibu

    Mechi ngumu kwa kila timu, ningependa kuona Dortmund ikishinda kuleta ushindani#meridianbettz

    Jibu

    Dortmund watakaa tu kwenye hii mechi Munich wapo vizur kombineshen ya gnarbry na lewandoski ni moto

    Jibu

    Bayern wanauchung wakufungw

    Jibu

    Dk 90 ndio muamuzi

    Jibu

    Mpira dk90

    Jibu

    Tusubili matokeo

    Jibu

    Ni mechi ngumu sana tutashuhudia upinzan wa haaland na lewandoski

    Jibu

    Kazi ipo hapo

    Jibu

    Hii n bonge la mechi kal sana 👍

    Jibu

    Bonge la mechi ambay nashindwag kujua nan atashinda

    Jibu

    Mi nasubiri matokeo tu maana nina mkeka wangu unapumua

    Jibu

    Safi

    Jibu

    sijui matokeo yalikuaje ya hii mechi…?

    Jibu

    Naisi ilikuwa apatoshi sio kwamechi hizo nazo ziona palikuwa apatoshi mtanange huo

    Jibu

    Ngoma ngumu hii

    Jibu

    Dakika za mwishoo tutajua mbabee wao

    Jibu

    Kocha kwa Dortmund alibugi sana kumfanyia sub Haaland mapema baada ya kusawazisha goli la pili

    Jibu

    Tusubili matokeo

    Jibu

    apo kazi ipo sizani kama bayern munich atakubali kupokea kichapo nyumbani kwake

    Jibu

    Tusubiri tuone matokeo

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.