Casemiro amemdokeza Marcus Rashford kuwa miongoni mwa wachezaji watano bora katika soka la Dunia na alikiri kushangazwa na jinsi mchezaji mwenzake wa Manchester United alivyo mzuri.

Rashford aliwekwa benchi kwa ajili ya safari ya United dhidi ya Wolves kwenye mechi yao ya jana kutokana na sababu za kinidhamu zilizoorodheshwa na kocha wake Ten Hag.
Lakini mshambuliaji huyo wa timu ya taifa ya Uingereza aliingia akitokea benchi na kufunga bao la ushindi katika ushindi wa 1-0 na kuendeleza wimbi lake la moto, ambalo limemfanya afunge mara tatu tangu arejee kutoka kwenye michuano ya Kombe la Dunia.
Rashford ana mabao 11 katika michuano yote msimu huu na Casemiro amefurahishwa na kile alichokiona tangu alipowasili kwa uhamisho wa pesa nyingi kutoka Real Madrid mwezi Agosti.

Casmeiro amesema; “Nitakuwa mkweli kwako, nilishangazwa sana na mchezaji ambaye Rashford na kwa maoni yangu hasa kumfahamu mchezaji nje ya uwanja, akifanya vizuri anaweza kuwa mmoja wa wachezaji watano bora Duniani.”
Ushindi wa United ulimaanisha wameanza 2023 katika nafasi nne za juu za Ligi ya Primia. Tottenham wanaweza kurudi nyuma mbele ya Mashetani Wekundu kwa kuwafunga Aston Villa siku ya leo, ingawa vijana wa Antonio Conte watakuwa wamecheza mchezo mmoja zaidi.

Vijana wa Erik ten Hag ndio wanaofuata uwanjani kucheza na Bournemouth siku ya Jumanne.

