Mshambuliaji Edinson Cavani amewasilisha maombi ya kuondoka Manchester United na kujiunga na Boca Juniors lakini pia kuwa karibu na familia yake.
Fowadi wa Manchester United Edinson Cavani amewaambia maafisa wa klabu anataka kuondoka klabuni msimu huu wa joto ili ajiunge na Boca Juniors, kulingana na ripoti.
Cavani alijiunga na Old Trafford kwa uhamisho wa bure kutoka PSG mwanzoni mwa kampeni.

Fowadi huyo mkongwe amefunga mabao matatu katika michezo yake mitatu iliyopita na klabu hiyo ina hamu ya kuongeza mkataba wake hadi msimu ujao, lakini mchezaji mwenyewe ameweka wazi nia yake baada ya kufanya mazungumzo na maafisa, inaripotiwa na Argentina Depo.
Cavani aliiambia klabu hiyo kuwa anataka kurudi Amerika Kusini ili kuwa karibu na familia yake, ripoti hiyo inaongeza kuwa alisema kwamba atakataa timu kadhaa za Brazil zinazotafuta saini yake ili tu ajiunge na Boca juniors.
Nafasi nyingine kwaajili yako, kasino mpya yenye hadhi ya kipekee inayokupa kila sababu ya kuwa mshindi katika kasino za Meridianbet, anza siku yako na njia rahisi ya kutengeneza mkwanja.



Adelta
Ni maamuzi mazuri kwake
aisha
Aende tuuu anapotaka
Lydia Emmanuel Magoti
Ahende tuuu
Saupha
Aendee tuuu
Magdalena
Cavani aende tu Wala hatustui
Khadija
Kula la kheri hilo aendako
warda
Aende tu