Chelsea FC Kupeleka Ofa ya £80m kwa Sancho.

 

Klabu ya Chelsea inatarajia kuipiku Manchester United katika usajili wa mshambuliaji wa Borussia Dortmund, Jadon Sancho katika majira ya kiangazi.

Kulingana na taarifa mbalimbali kutoka nchini England, Chelsea ipo tayari kupeleka ofa ya £80m pale Signal Iduna Park kwaajili ya kupata huduma za mchezaji huyo.

 

Jarida la The Sun liliandika mchezaji huyo yupo tayari kuondoka Dortmund mwishoni mwa msimu wakati akitaka kurejea katika ligi ya Premia na Chelsea wanaongoza katika kinyang’anyiro hicho.

Klabu ya Manchester United pia walikuwa wanahusishwa na mshambuliaji huyo lakini hawakuwa tayari kutoa kitita cha £117m kilichotakiwa na Dortmund.

Sancho amefunga magoli 8 na kutoa assist 11 katika michezo 25 aliyocheza Bundesliga msimu huu pamoja na kuanza vibaya mwanzoni mwa msimu, Tuchel anatajwa kuwa anamhusudu kinda huyo.


UNAWEZA KUWA MILIONEA WAKATI WOWOTE!

Zungusha na ushinde mkwanja wako papo hapo baada ya mzunguko kukamilika. Ni kugusa tu 🤑.

kane, Kane Aweka Wazi Maazimio Yake Kucheza UEFA., MeridianbetBASHIRI SASA

Acha ujumbe