Dilunga Mchezaji Bora Mwezi October.

 

Kiungo mshambuliaji wa Simba SC, Hassan Dilunga, amekabidhiwa tuzo ya mchezaji bora wa Oktoba wa mashabiki (Emirate Aluminium Simba Fans Player of the Month) na wadhamini Emirate Aluminium ACP.

 

Dilunga (2249) amewapiku viungo wenzake Rally Bwalya (2199) na Sadio Kanoute (376) ambao waliingia fainali ya kinyang’anyiro hicho. Emirate imemkabidhi kitita cha Sh 2,000,000 na ngao kama sehemu ya zawadi baada ya kunyakua tuzo hiyo.

Meneja Masoko na Mahusiano wa Emirate Aluminium ACP, Issa Maeda amesema ni tuzo kubwa ambayo inatolewa katika ukanda huu wa Afrika Mashariki na Kati na haijawahi kutolewa kabla.

β€œEmirate Aluminium ACP tunatoa kiasi kikubwa cha fedha kwa mchezaji bora wa Simba, ni kikubwa mara mbili zaidi ya msimu uliopita, hata mchezaji bora wa ligi hapati kama hiki nadhani itaongeza chachu kwa wachezaji kuendelea kufanya vizuri,” amesema Maeda.

Kwa upande wake Dilunga amewashukuru mashabiki kwa kumpigia kura nyingi na wamemfanya kujiona ana deni kubwa na ataendelea kujituma kama sehemu ya kurejesha shukrani kwao.

β€œKwanza nawashukuru mashabiki kwa kunipigia kura nyingi, naishukuru familia yangu na marafiki wa karibu kwa kuhamasisha mpaka nikapata tuzo hii, kiukweli najiona nina deni kubwa na nitaendelea kupambana kupata tena na tena,” amesema Dilunga.


MKWANJA WA KUSHATO NA AURORA BEAST HUNTER!

Mkwanja umetema ndani ya kasino za meridianbettz, Mchezo maridhawa wa Aurora Beast Hunter unakupa nafasi sawa ya ushindi leo hii, kila mzunguko una nafasi ya kuibuka mshindi, na mkwanja wako unaupata kila mzunguko utakapo kamilika.

tetesi, Tetesi za Soka Barani Ulaya., Meridianbet

CHEZA HAPA

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.