Everton wako tayari kuwakaribia Atalanta kufanya mazungumzo ya kumnunua mshambuliaji wa Colombia Duvan Zapata ambaye anashiriki katika Ligi ya Hispania.

Waamuzi watafanyia kazi mkataba huo na Everton iliyo wazi kwa mkopo na pendekezo la kipengele cha chaguo. Atalanta itakuwa wazi tu kujadili uhamisho wa kudumu wa Zapata, kama mambo yalivyo.
Everton ambayo ipo chini ya kocha mkuu Frank Lampard bado ina hali tete katika msimamo wa ligi kuu ya Uingereza baada ya kuwa na mwendelezo mbaya wa matokeo wanayoyapa.

Timu hiyo ipo nafasi ya 19 ambayo ni ya pili kutoka mwisho baada ya kucheza michezo yake 19. Wameshinda mechi tatu pekee, sare sita na kupoteza michezo kumi mpaka sasa na kujikusanyia alama 15.
Timu hiyo ya Uingereza wanaamini wakifanikiwa kumsajili Zapata ataenda kuwasaidia katika eneo lao la ushambuliaji kwani mpaka sasa wanadaiwa mabao 11.

