Mkurugenzi wa michezo wa Bayern Munich, Max Eberl, Jumatatu alithibitisha kuwa klabu iko kwenye mazungumzo ya kuongeza mkataba wa Harry Kane. Mshambuliaji huyo wa England mwenye umri wa miaka 32, aliyejiunga na Bayern mwaka 2023, ana mkataba unaoendelea hadi mwaka 2027.

“Tunaongea na Harry, mazungumzo yanaendelea,” Eberl alisema wakati wa tukio la Bundesliga mjini Frankfurt. “Kila mtu anajua kuwa kufikia wakati fulani uamuzi lazima ufanywe,” aliongeza.
Mkurugenzi Mtendaji wa klabu, Jan-Christian Dreesen, pia alisema Harry ana imani kubwa nao na anajisikia vizuri sana akiwa Munich. Yeye na familia yake wameshazoea mazingira, hivyo hawana sababu yoyote ya kuharakisha.
Baada ya muda mrefu bila kutwaa taji la timu, Kane alivunja ukame huo mwaka 2025 pale Bayern walipotwaa ubingwa wa Bundesliga.
Msimu huu, Bayern wako mbele kwa pointi nane kileleni mwa ligi na wanashika nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya yenye timu 36.
Meridianbet inakwambia kuwa endelea kubashiri hapa kwani ODDS KUBWA na machaguo zaidi ya 1000 yapo hapa. Ingia kwenye akaunti yako na uanze safari yako ya ushindi sasa.


