Kocha mkuu wa PSG, Christophe Galtier amesema kuwa Kylian Mbappe alikabiliwa na uchovu wa misuli katika ushindi wa Paris Saint-Germain dhidi ya Lorient, na kocha huyo ameondoa hofu juu ya utimamu wa mshambuliaji huyo kabla ya Kombe la Dunia.
PSG, walishinda kwa mabao 2-1 huku bao la ushindi likifungwa na Danilo Pereira na kuwafanya wawe kileleni kwa Ligue 1 kwa pointi 5 mbele wakifuatiwa na Lens wenye pointi 33.
Galtier alimfanyia mabadiliko Mbappe baada ya kuonekana kuwa na uchovu wa misuli kutoka kwenye mechi siku ya Jumatano dhidi ya Juventus lakini hana wasiwasi kuhusu hali yake kwani anaweza kurejea uwanjani muda wowote.
Mpaka sasa Ufaransa tayari itawakosa Paul Pogba na N’Golo Kante kwa eneo la kiungo kuelekea Kombe la Dunia, wakati Karim Benzema amekosa mechi kadhaa za Real Madrid katika msimu ambao ni majeruhi, ikiwa ni pamoja na kukutana na Rayo Vallecano.
Galtier aliiambia Amazon Prime Video: “Sio jambo kubwa , tuliona habari kuhusu Karim lakini hakuna jambo zito kwa Kylian.”
Aliongeza kwa kusema kuwa Mbappe alifanya juhudi na ni bora kuomba kuondoka kuliko kujihatarisha kubaki uwanjani, au kuwa uwanjani na kukosekana kabisa. Lakini hakuna hakuna tahadhari katika eneo maalum, ni uchovu unaohusishwa na mlolongo wa mechi.
PSG hawakuwa na Lionel Messi dhidi ya Lorient, ingawa anatarajiwa kurejea kabla ya mapumziko ya Kombe la Dunia.
Ulishawahi kuwaza kuwa rubani wa maisha yako!! Kuwa rubani wa mchezo pendwa wa Aviator wa kasino mtandaoni. Aviator bonanza inazidi kutoa michongo ya mkwanja kwenye nyumba ya mabingwa. Unarusha ndege yako na unashinda, kuwa rubani wa kujivunia kwa kuibuka na mkwanja leo.
BONYEZA HAPA