Galtier Amesema Tusi la Kihispania Lilimpa Ramos Kadi Nyekundu

Kocha mkuu wa Paris Saint German Christophe Galtier amethibiisha kuwa kutukanwa kwa Kihispania ndio ilikuwa sababu kuu ya beki wake Sergio Ramos Kupewa kadi nyekundu hapo jana kwenye mchezo dhidi ya Reims.

 

Galtier Amesema Tusi la Kihispania Lilimpa Ramos Kadi Nyekundu

Christophe na vijana wake walikuwa ugenini hapo jana na walitoa sare ya bila kufungana, hivyo ikiwa ni sare ya pili mfululizo baada ya kutoa nyingine kwenye mchezo uliopita wa ligi ya Mabingwa dhidi ya Benfica.

Ramos alipata kadi mbili za njano baada ya muda mfupi kabla ya mapumziko na kuwaacha Psg wakiwa kumi uwanjani huku kadi hiyo ikitokana na kugombana vikali na mwamuzi wa mchezo huo.

Galtier Amesema Tusi la Kihispania Lilimpa Ramos Kadi Nyekundu

Ramos ambaye ni Mhispania ametimuliwa nje kwa mara ya 21 katika maisha yake ya soka akiwa Laliga pamoja na Ligue 1. Akizungumza baada ya sare hiyo, ambayo inaifanya Psg iiache Marseille kwa pointi tatu kileleni, kocha huyo alisisitiza kuwa anaamini kuwa beki wake Ramos hakukusudia kumkera Gaillouste.

“Ninamfahamu vyema Sergio Ramos, sina uhakika kuwa tusi lililotoka lilielekezwa kwa mwamuzi,” Galtier alisema.

Galtier Amesema Tusi la Kihispania Lilimpa Ramos Kadi Nyekundu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.