Klabu ya Azam FC yazamishwa shimoni na Al Akhdar baada ya kutandikwa mabao 3-0 ugenini katika mchezo wa michuano ya Kombe la Shirikisho Barani Afrika uliofanyika majira ya saa 2:00.

Mabao hayo yote yalifungwa katika dakika 45 za kwanza za mchezo ambapo mabao hayo yalidumu hadi dakika 90 za mchezo na ndani ya dakika 41 yalipatikana magoli mawili huku dakika za lala salama Al Akhdar wakipata mkwaju wa penati ambao unaokolewa na golikipa wa Azam
Wanalambalamba mchezo wao wa kwanza wameanzia ugenini dhidi ya timu kutoka Libya mambo yamekuwa magumu sana, lakini kuna nafasi nyingine ya pili ya kusahihisha pale alipokosea.

Mechi ya marudiano kati yao na Al Akhdar itakuwa ni tarehe 16 ambapo Matajiri wa Chamazi watahitaji kupindua meza endapo kama itawezekana ili waweze kusonga mbele kwenye hatua inayofuata ya michuano hii.

