Chanzo cha habari cha Star siku ya jana kimeripoti kwamba Pep Guardiola ambaye ni kocha wa klabu ya soka ya Manchester City atakuwa anawawinda kwa ukaribu kabisa wachezaji wawili wa klabu ya soka ya Lyon ya huko Ufaransa ambao ni Luca Tousart na Tanguy Ndombele.
Hili litafanyika wakati ambapo timu hiyo itakuwa ikisafiri kuelekea Etihad siku ya Jumatano na wachezaji hawa wawili wa Ufaransa ambao wote wana umri wa miaka 21 wamekuwa kivutio kwa klabu zingine za huko majuu.
Ya Bruyne
Pia, Pep Guardiola amesema kwamba mchezaji Kevin De Bruyne mwenye umri wa miaka 27 hana sheria inayomkaba kwenye mkataba wake baada ya kusema kwamba kiungo huyo anaweza kuuzwa kwa kitita cha £223m!
Wakati huo huo, Kelvin de Bruyne anatarajiwa kurejea kukipiga dimbani kwa mara ya kwanza baada ya kuwa majeruhi na hii itakuwa ni wakati wa mtanange utakaopigwa mnamo tarehe 11 mwezi wa 11. Mchezaji huyo alitolewa kwenye mashindano baada ya kuumia mguu wake wa kulia akiwa dimbani.


Povel
Kocha mzuri sana
Fatina mfingi
Ni kocha bora sanaa