Hatimaye ile tarehe 26 iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu ikafika bhana ambapo kulikuwa na mchezo mkali sana kule LALIGA ambao ulikuwa ni EL Clasico kati ya Real Madrid vs Barcelona Yamal akipeleka moto haswa.
Mchezo huo ulipigwa majira ya saa 4 usiku kwa saa za Afrika Mashariki, katika dimba la Santiago Bernabeu ambapo Barcelona chini ya kocha mkuu Hans Flick wakiibamiza Madrid ya Ancelotti bila huruma nyumbani kwao.
Ni mechi ambayo baadhi ya watu wengi waliaamini kuwa Real anaenda kushinda kutokana na usajili mkubwa ambao ameufanya ikiwa ni pamoja na kumleta mshindi wa Kombe la Dunia 2018 bwana mdogo Kylian Mbappe lakini mambo hayajakuwa kama ilivyotarajiwa hapo jana mpaka dakika 90 kukamilika.
Walienda mapumziko wakiwa 0-0 na ndipo sasa waliporeje mechi ikawa ni kali haswa kwani Robert Lewandowski alianza kufungua ukurasa wa mabao dakika ya 54 na 56, lakini pia baadae dakika ya 77 Yamal aliingia kambani na kufanya mabao kuwa 3 na mwisho kabisa Raphina alimaliza kwa kufunga la 4.
Mbappe alijitahidi sana lakini walikuwa wamenasa kwenye mtego wa Barcelona baada ya kucheza OFFSIDE 12 na kuwafanya washindwe kufurukuta wakiwa nyumbani licha ya Vini, Bellingham, wote kuwepo dimbani hakuna kilichobadilika.
Baada ya ushindi huo sasa vijana wa Catalunya wanasalia kileleni kwenye msimamo wa ligi wakiwa na pointi zao 30, huku Madrid akiwa wa pili na pointi zake 24 baada ya kupoteza mechi yake ya kwanza hapo jana.
This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.
Strictly Necessary Cookies
Strictly Necessary Cookie should be enabled at all times so that we can save your preferences for cookie settings.
If you disable this cookie, we will not be able to save your preferences. This means that every time you visit this website you will need to enable or disable cookies again.