Xavi Awapa Adhabu Wachezaji wa Barcelona Baada ya kutoa Sare ya 1-1 na Espanyol

Sare ya jana ya 1-1 dhidi ya Espanyol kwenye dabi ya Catalan ilikuwa matokeo ya kukatisha tamaa kwa Barcelona na kocha mkuu Xavi Hernandez.

 

xavi

Akiwa ameongoza mapema kupitia kwa Marcos Alonso, mchezaji huyo wa zamani wa Chelsea alitoka shujaa hadi kuwa mzembe huku akisababisha mkwaju wa penati wa dakika za lala salama, ambao ulimruhusu Joselu kusawazisha upande wa ugenini na kunyakua pointi isiyo na thamani.

Kwa matokeo hayo, Barcelona (Blaugrana) bado wanaongoza La Liga, lakini pengo lao dhidi ya Real Madrid wanaoshika nafasi ya pili limefutika. Sasa, tofauti ya mabao ya kufunga na kufungwa tu ndio inamfanya Barca kuongoza Ligi.

Kama Barcelona wangeshinda kwenye derby ya jana, wachezaji wangezawadiwa na Xavi siku ya mapumziko ya Siku ya Mwaka Mpya, kama ilivyo kwa Diario AS. Badala yake, kikosi kitaagizwa kwenda Ciutat Esportiva saa 18:00CET kufanya mazoezi ya ziada.

Xavi anatumai kuwa mazoezi ya ziada yatakuwa ya manufaa huku timu ikijiandaa kumenyana na Primeira Federacion CF Intercity kwenye Copa del Rey Jumatano jioni (michezo saa 21:00CET).


Bashiri na kitochi au bila bando mechi hii, Bonyeza hapa kutazama ODDS kubwa na bomba kupitia machaguo spesho ya meridianbet ili kuingia mchezoni. Pia ukibashiri na kitochi kwa dau la TZS 1,000/= Unaweza kuibuka mshindi wa MBUZI WA KITOWEO CHA SIKUKUU, kila wiki Ijumaa.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.