Mbappe Mchezaji Mdogo Zaidi Kufikisha Mabao 10 Kombe la Dunia

Kylian Mbappe amekuwa mchezaji mwenye umri mdogo zaidi kufunga mabao 10 kwenye Kombe la Dunia akiwa njiani kuifikisha Ufaransa sawa na Argentina kwenye fainali ya Qatar 2022 hapo jana.

 

Mbappe Mchezaji Mdogo Zaidi Kufikisha Mabao 10 Kombe la Dunia

Mshambuliaji huyo aliipa Les Bleus matumaini kwa mkwaju wa penalti katika dakika ya 80, kabla ya voli ya ajabu kutokea sekunde 97 baadaye kwenye Uwanja wa Lusail, ambapo mkwaju wa Lionel Messi na bao la Angel Di Maria vilionekana kuwafanya Argentina wadhibiti.

Akifikisha mabao 11 katika Kombe la Dunia, Mbappe ndiye mchezaji mwenye umri mdogo zaidi kufikisha idadi hiyo maradufu kwenye fainali akiwa na  umri miaka 23 siku 363, akivuka rekodi ya Gerd Muller (miaka 24, siku 226).

Mbappe Mchezaji Mdogo Zaidi Kufikisha Mabao 10 Kombe la Dunia

Nyota huyo wa Paris Saint-Germain pia amekuwa mchezaji wa tano kufunga mara tatu katika fainali ya Kombe la Dunia, akiwa pia amefunga dhidi ya Croatia katika mechi ya 2018, pamoja na Vava, Geoff Hurst, Pele na Zinedine Zidane.

Acha ujumbe