Kiungo mshambuliaji wa Geita Gold, Kelvin Nashon amefunguka kuwa ubora wa kikosi cha Simba ndio uliopelekea kupoteza kwa mabao mengi.
Nashon amesema kuwa waliingia na mpango wao wa mechi ambao ulizidiwa na ubora waliokuwa nao wachezaji wa Simba na kupelekea kupoteza mchezo huo.
“Kwanza tunashukuru mchezo umemalizika salama japo tumepoteza kwa idadi kubwa ya magoli lakini ndio mpira.
“Sisi tuliingia na mpango wetu wa mechi lakini zimefeli kwahiyo Simba wameonekana wapo juu zaidi yetu ila kuna baadhi ya makosa madogo madogo yamefanya tumepoteza kwa mabao mengi.”