Guardiola : Silva ni Mchezaji Aliyekamilika.

 

Kocha wa Manchester City, Pep Guardiola amemtaja Bernardo Silva kama mchezaji bora baada ya kufunga mabao mawili katika ushindi wa 5-0 dhidi ya Sporting Lisbon hapo jana.

 

City wamekaribia kufuzu robo-fainali kwa kugawa kichapo kikubwa zaidi kwa Sporting wakiwa nyumbani katika mashindano ya Ulaya, huku wakisisitiza hadhi yao kama vinara wa Ligi ya Mabingwa.

Silva ambaye ni mchezaji wa zamani wa Benfica, alicheza katika mji wake wa nyumbani, akifunga bao la ajabu la nusu voli lililotinga langoni na kuifanya City kuwa mbele kwa mabao 2-0, kabla ya juhudi zake kufanya matokeo kuwa 4-0 hadi mapumziko.

“Siku zote mimi humwambia ‘wewe ni mchezaji kamili’,” Guardiola alisema. “Pamoja na mpira, ni mchezaji wa kipekee, lakini huwa namwambia lazima uende kushinda michezo, uwe na uwezo wa kufanya hivyo. Ana mbinu, kila kitu.

“Huu ulikuwa mji wake wa asili, na anapenda kurejea hapa. Bila shaka, ni mchezaji wa zamani wa Benfica, hivyo hii ilikuwa ni siku maalum kwake usiku wa leo.” aliongeza Guardiola.


KASINO YA MTANDAONI: EMOTICOINS SABABU YA KUVUNA ZAIDI.

Haijawahi kuwa rahisi hivi kwenye safari yako ya kuvuna mkwanja, kasino maridhawa ya meridianbettz inakuletea mchezo wa Emoticoins unaokupa nafasi ya kufanya safari yako kuwa rahisi zaidi. Wakati ni wako nafasi ni yako na Emoticoins.

senegal, Senegal Mabingwa AFCON 2021., Meridianbet

CHEZA HAPA.

Acha ujumbe