Liverpool Wanakaribia Kuongeza Mkataba wa Ibrahima Konate

Paris Saint-Germain, Real Madrid na Inter Milan zote zilikuwa zikimfuatilia beki wa kati wa Liverpool Ibrahima Konate.

Liverpool Wanakaribia Kuongeza Mkataba wa Ibrahima Konate

Ibrahima Konaté yuko karibu kuongeza muda wa kukaa kwake Liverpool. Liverpool wanakaribia kufikia makubaliano ya mkataba mpya na beki wao nyota Ibrahima Konate, kulingana na mtaalamu wa masuala ya usajili Fabrizio Romano.

Mkataba wa sasa wa Mfaransa huyo unatarajiwa kuisha majira haya ya joto, na kulikuwa na hofu kubwa kwamba angeondoka bure mwishoni mwa mwaka huu.

Mabingwa wa Ligue 1 PSG, wababe wa La Liga Real Madrid na vinara wa Serie A Inter Milan wote walihusishwa na nia ya kumsajili mchezaji huyo wa zamani wa RB Leipzig kwa uhamisho wa bure.

Hata hivyo, timu hizo pamoja na nyingine zinatarajiwa kukosa huduma zake, kwani sasa Konate yuko karibu kukubaliana masharti mapya na Liverpool.

Liverpool wamekuwa wakitamani sana kumuongezea mkataba Konate, lakini mazungumzo yalikuwa yamesimama katika miezi ya hivi karibuni.

Liverpool Wanakaribia Kuongeza Mkataba wa Ibrahima Konate

Baada ya kufikia hatua kubwa katika mazungumzo, sasa Konate anaonekana yuko tayari kusaini mkataba mpya na mabingwa watetezi wa EPL.

Romano alisema: “Mazungumzo haya yanaelekea katika hatua za mwisho. Makubaliano kati ya Konate na Liverpool yanakaribia sana, yako karibu kukamilika. Bado hayajakamilika rasmi, na tunapaswa kusubiri hadi mwisho kabisa kabla ya kusema yamekamilika, kwa sababu kwa wachezaji huru na muhimu kama Konate, mambo yanaweza kubadilika kwa haraka.”

Lakini kwa sasa, mazungumzo yanaendelea vizuri sana ili kufanikisha mkataba mpya.

Mshahara karibu umekubaliwa, muda wa mkataba bado unajadiliwa, na kuna baadhi ya vipengele vinavyohitaji kufafanuliwa, lakini pande zote mbili ziko karibu sana kufikia makubaliano.

Habari hizi zitakuwa faraja kwa Liverpool, ambao wamekuwa na msimu wa pili usioridhisha chini ya kocha Arne Slot.

Liverpool Wanakaribia Kuongeza Mkataba wa Ibrahima Konate

Liver wako nyuma kwa pointi 21 dhidi ya vinara wa ligi Arsenal wakiwa na mechi saba zilizobaki, huku pia wakipoteza 2-0 dhidi ya PSG katika mchezo wa kwanza wa robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Jumatano usiku.

Shinikizo linaongezeka kwa Slot kurejesha kiwango cha timu, na bado haijulikani kama ataendelea kuwa kocha wa Liver kufikia msimu wa 2026-27.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.