CONMEBOL Yamuunga Mkono Infantino Kuendelea na Urais FIFA Kwa Muhula wa Nne

Shirikisho la Soka la Amerika Kusini, CONMEBOL, limetangaza kumuunga mkono Rais wa FIFA, Gianni Infantino, iwapo ataamua kugombea tena nafasi hiyo kwa muhula wa nne.

CONMEBOL Yamuunga Mkono Infantino Kuendelea na Urais FIFA Kwa Muhula wa NneKupitia taarifa iliyotolewa Alhamisi, baraza la CONMEBOL limesema kwa kauli moja limeonyesha uungwaji mkono wake kwa kiongozi huyo mwenye umri wa miaka 56, hata kabla hajathibitisha rasmi nia yake ya kugombea muhula wa 2027–2031.

Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa

Rais wa CONMEBOL, Alejandro Dominguez, amempongeza Infantino kwa mchango wake katika maendeleo ya soka duniani na hasa katika ukanda wa Amerika Kusini.

CONMEBOL Yamuunga Mkono Infantino Kuendelea na Urais FIFA Kwa Muhula wa Nne“Rais Gianni Infantino, tunakushukuru kwa kujitolea kwako kuendeleza soka la Amerika Kusini na kwa uongozi wako katika ngazi ya kimataifa,” amesema Alejandro Dominguez.

Ameongeza kuwa, Tunathamini kwa dhati ukaribu wako na ukanda wetu pamoja na maono yako ya kuendelea kukuza mchezo wa soka duniani kote.”

CONMEBOL Yamuunga Mkono Infantino Kuendelea na Urais FIFA Kwa Muhula wa NneCONMEBOL inakuwa shirikisho la kwanza kutangaza wazi kumuunga mkono Gianni Infantino kwa uchaguzi ujao. Infantino alichukua madaraka mwaka 2016 akimrithi Sepp Blatter, na alichaguliwa tena bila kupingwa mwaka 2019 na 2023.

CONMEBOL Yamuunga Mkono Infantino Kuendelea na Urais FIFA Kwa Muhula wa NneKatika kipindi chake, ameendeleza upanuzi wa mashindano ya FIFA, ikiwemo kuongeza timu hadi 48 kwenye Kombe la Dunia na 32 kwa mashindano ya wanawake, ingawa pia amekumbana na ukosoaji kuhusu masuala ya uongozi na msongamano wa kalenda ya michezo.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.