Kiungo mkabaji wa Simba SC, Jonas Mkude, amechaguliwa mchezaji bora wa mashabiki wa mwezi Desemba (Emirate Aluminium ACP Simba Fans Player of the Month).
Mkude amewashinda walinzi wawili wa kati Joash Onyango na Henock Inonga Baka ambao aliingia nao fainali ya kinyangโanyiro hicho.
Katika mwezi Desemba, Jonas amecheza mechi nne kati ya tano akihusika katika upatikanaji wa mabao mawili (assist) huku akionyesha kiwango bora.
Mchezaji huyo atakabidhiwa pesa taslimu Sh 2,000,000 pamoja na tuzo kutoka kwa Wadhamini Emirate Aluminium ACP kama sehemu ya zawadi.
Mchanganuo wa kura ulivyokuwa:
Mkude kura 2397 (43.93%)
Onyango kura 2393 (43.85%)
Inonga kura 667 (12.22%)
Una Kila sababu ya kufurahia wiki yako na kutengeneza mwaka huu uwe wa faida zaidi katika kasino zetu za mtandaoni za meridianbettz. Mchezo wa Zeus Ancient Fortunes unakuongoza kutekeleza hilo.