Licha ya David Moyes kuugua Covid-19, kocha huyo raia wa Scotland atasimamia mechi itakayowakutanisha West Ham United na Wolves katika Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) mnamo Septemba 27, 2020 uwanjani London Stadium akiwa nyumbani kwake.
Haya ni kwa mujibu wa kocha msaidizi wa West Ham, Alan Irvine ambaye amethibitisha kuwa Moyes kwa sasa amejitenga nyumbani katika juhudi za kudhibiti msambao wa virusi vya corona.

Baada ya kupatikana na corona, Moyes kwa pamoja na wanasoka Issa Diop na Josh Cullen walilazimika kuondoka uwanjani London Stadium haraka iwezekanavyo kabla ya mechi iliyowakutanisha na Hull City kwenye Carabao Cup kupigwa mnamo Septemba 22, 2020.
Licha ya Moyes kufichua mpango wake wa kufanyia kazi nyumbani kwa siku kadhaa zijazo, Irvine ndiye atakuwa kwenye eneo la kocha kwa upande wa West Ham katika mechi zijazo.
“Kila kitu tutakachofanya uwanjani kuanzia sasa kitaidhinishwa na Kocha. Sisi uwanjani London Stadium tutasalia tu kutekeleza maagizo atakayokuwa akitoa akiwa nyumbani kwake,” akatanguliza Irvine.

“Hata hii taarifa rasmi tunayoitoa sasa kwa vyombo vya habari imeandaliwa na kocha huyo akiwa nyumbani. Atasalia kufanyia kazi nyumbani hadi atakapopona. Mimi na wenzangu kwenye benchi ya kifundi ni wajumbe tu,” akaongeza.
Kwa mujibu wa Irvine, Moyes na wachezaji Diop na Cullen hawakuonyesha dalili zozote za corona kabla ya kufanyiwa vipimo vya afya na kupatikana na ugonjwa wa Covid-19.
FURAHIA KASINO YA MTANDAONI
Tembelea ardhi ya maajabu ushangazwe na mengi ikiwa ni pamoja na urahisi wa kujipatia utajiri kupitia Kasino ya Meridianbet.


Saupha mohamed
Duuu corona sio poa
farida ahmadi
Duh nouma corona inajua kuitikisa dunia
Tatu
Ni kocha anaependa kazi yake
Mwajumah
Duuh hii corona sio poa kabisa
Khadija
Corona noma sana
Agness
Oojamani mungu amsaidie atoke caratin
Fatina mfigi
Corona tuache kidog
aisha
Moyes anaipenda sana kazi yake na ndio maana anafanya yote hayo
Lydia Emmanuel Magoti
Duu sio poa
Zeiyana
Korona himekua hatari jamani daah..!
Venerose
Corona ni janga la taifa
Shani
Corona ni shida
Sadick
Ni kama hana imani na wasaidizi wake! Nadhani anataka kuona kila kitu kinakwenda sawa#meridianbettz
Hidaya
Corona bado ni tishio
Hopemwaikuka
Fresh tu
Caroline
Safi sana ata Kama kuna Corona lakini lazima maisha yaendelee
Elika
Dah sio poa hii corona
Amiri
Duh nomaa san
Nasra
Hatarii hii
Gabriel
Corona ni janga
Adelta
Coronavirus sio poa
lombo
vzr
Rehema
Corona sio poa
Ernest
Westham watamuwakilisha vizuri Kocha wao
Issa
Corona ni shida
Flomena
Duuu huuu Ugonjwa bado Ni hatari sana
Fatuma kasomo
Nomaa
Janeflora malisa
Safi
Neema
Corona ni noma
Samiah
SAfi
Latifa juma mohamed
Corona ni shida!
David Pere
Ni kama hana imani na wasaidizi wake! Nadhani anataka kuona kila kitu kinakwenda sawa
Sauda
Moyes anajituma sana
Asia Abdy
Safii anajitumaa
felister
anaipenda kazi yake
Rose kapinga
Kocha mwenye kipaji chake hakiharibiki kitu!!
Sabrina
Safi sana moyes
Theckla
Jamani corona binafsi nakuombea apone na arejee kwenye majukum yake
magdalena
huu ugonjwa umekuwa tishio kubwa sana Mungu tu atusimamie
Povel
Covid 19 ni janga la dunia
Dorophina
Corona inatuharibia radha ya mpira