Kiungo wa Klabu ya Manchester United, Paul Pogba ameweka wazi hisia zake baada ya kukubali kichapo cha 4-2 walipotembelea uwanja wa King Power Stadium hapo jana.

Pogba amesema timu yao imestahili kupoteza mchezo huo baada ya timu kucheza chini ya kiwango kupoteza ubora wao na kuruhusu Leicester City kucheza zaidi.
“Niwe mkweli, tumekuwa tukicheza hivi kwa muda mrefu sasa” Pogba aliiambia BBC baada ya mchezo hapo jana.
“Hatujajua tatizo bado, tunaruhusu magoli rahisi, magoli ya kijinga. Tunahitaji kukomaa, kucheza kwa umakini na ubunifu.
“Tunahitaji kutafuta kitu, tunahitaji kubadilika.”
United wanashika nafasi ya tano katika msimamo wa ligi kuu wakiwa hawajapata ushindi katika michezo mitatu mfululizo ya ugenini baada ya kuanza vizuri msimu.
Fanya wiki yako iwe ya kuvutia zaidi, tunaelekea Los Angeles kutengeneza mkwanja na kasino maridhawa ya LA Rouge kutoka katika kasino za mtandaoni za meridianbettz, Fursa ya kufurahi huku unajaza pochi yako.

CHEZA HAPA

