Ruben Amorim amekiri kuwa timu yake ya Manchester United ilikuwa ikijaribu tu “kuhimili presha” kipindi cha pili baada ya kuwekwa chini ya shinikizo kubwa na Newcastle United.

Mashetani Wekundu walipata bao la uongozi pale mpira wa mkwaju mkali wa Patrick Dorgu ulipopita kwa Aaron Ramsdale. Bao hilo hatimaye lilitosha kuwapatia wenyeji pointi zote tatu, ingawa walilazimika kujilinda kwa nidhamu kubwa ili kuhakikisha wanadumisha ushindi huo.
Licha ya Newcastle United kutawala umiliki wa mpira kwa sehemu kubwa ya kipindi cha pili, walishindwa tena kuvunja safu imara ya ulinzi na wakaondoka Old Trafford wakiwa wamepata tena kipigo cha ugenini kwenye Ligi Kuu.
The Magpies wamekusanya pointi sita tu kati ya 27 zinazowezekana wakiwa ugenini kwenye ligi msimu huu, na ni Wolves pekee walioko mkiani mwa msimamo wa ligi wenye ushindi mdogo zaidi wa ugenini kuliko kikosi cha Eddie Howe.



