Sarri Akataa Kuinoa Nottingham Forest

Ripoti za Italia zinadai kuwa Nottingham Forest ilimpa Maurizio Sarri mkataba wa miaka mitatu baada ya kujiuzulu kutoka Lazio, lakini akawakataa.

Sarri Akataa Kuinoa Nottingham Forest

Kocha huyo alijiuzulu mnamo Machi 13 kufuatia kushindwa mara nne mfululizo katika mashindano yote. Pia meridianbet inatoa michezo ya kasino ya mtandaoni kama vile, Aviator, poker, Roullette, sloti na mingine kibao. Ingia meridianbet na ucheze sasa.

Kulingana na mtaalam wa uhamisho wa Sportitalia Alfredo Pedullà, siku chache baada ya tukio hilo, Nottingham Forest iliwasiliana na wawakilishi wa Sarri kuuliza kama angependa kuchukua nafasi mpya mara moja kwenye Ligi Kuu.

Klabu hiyo inatatizika kwa sasa kufuatia adhabu ya pointi nne kwa ukiukaji wa utendaji kazi wa Financial Fair Play na matokeo duni chini ya Nuno Espirito Santo.

Sarri Akataa Kuinoa Nottingham Forest

Walikuwa tayari kumpa Sarri kandarasi ya miaka mitatu, na kuahidiwa kuimarisha kikosi katika majira ya joto. Lakini, kocha huyo hakupendezwa na atachukua miezi michache kabla ya kuamua hatua yake inayofuata.

Tayari amekuwa akihusishwa mara kwa mara na kazi ya Fiorentina, ambayo ingemruhusu kurejea nyumbani.

 

Acha ujumbe