Klabu ya Simba SC imemtambulisha kocha mpya wa magolikipa, Tyron Damos kuchukua nafasi iliyoachwa na aliyekuwa kocha wa klabu hiyo Milton Nienov.
Tyron amejiunga na Simba SC akitokea Afrika Kusini ambako amewahi kucheza katika nafasi hiyo katika klabu ya Bidvets Wits kabla ya kuwa kocha wa magolikipa katika timu hiyo baada ya kustaafu.
Tyron, 43 ambaye ni raia wa Afrika Kusini ana elimu ya ukocha leseni C ya Shirikisho la Soka Afrika (CAF), Kozi ya ukocha wa magolikipa kutoka Shirikisho la Soka Uholanzi na Afrika Kusini.
Pia amewahi kuzifundisha timu za TS Galaxy na Chippa United za ligi kuu ya afrika Kusini. Na sasa amejiunga rasmi na kuanza majukumu yake akiwa na Simba SC.
Unaweza kujishindia mamilioni katika kasino yako pendwa ya meridianbettz, mchezo wa Agent Jane Blonde Return ni moja ya michezo inayopendwa kwasasa huku ikiwafanya wachezaji kuwa mamilionea kila siku. Unasubiri nini! ungana na Agent Jane Blonde akufanye milionea.
CHEZA HAPA