Tetesi zinasema Manchester City wameingia kwenye kinyang’anyiro cha kumsaka kiungo wa kati wa Bayern Munich.
Manchester United wamesitisha kwa muda biashara ya kuwahamisha wachezaji huku wakijaribu kusaini mkataba na winga wa Borussia Dortmund na England Jadon Sancho, 20.
Watford wako tayari kudai rekodi ya garama ya zadi ya pauni milioni 40 kwa winga Msenegal Ismaila Sarr, 22, huku Liverpool na klabu nyingine za Ulaya zikitangaza nia yao ya kumchukua.
Tetesi zinasema Sarr amewaambia waandishi wa habari nchini Senegal kwamba “kile mtu angependa ” kuchezea Liverpool.

Roma wanaweza kumbadilisha kiungo wa kati Mguinea Amadou Diawara mwenye umri wa miaka 23 na kiungo wa kati Arsenal Lucas Torreira ambaye ni raia wa Uruguay mwenye umri wa miaka , 24.
Tetesi zinasema Valencia wamezifahamisha klabu za Ligi ya Epl kuwaweka sokoni wachezaji wao wote isipokua mmoja ili kupata pesa.
Jack Grealish atafanya mazungumzo kadhaa na Mkurugenzi mkuu wa Aston Villa Christian Purslow juu ya kurejea kwake kutoka mapumzikoni , huku Manchester United wakiwa bado wanania na kiungo huyo wa safu ya kati mwenye umri wa miaka 24 .

Benfica wanaongoza katika mbio za kumsaini beki wa zamani wa Tottenham Jan Vertonghen na Mbelgiji huyo mwenye umri wa miaka 33- anaweza kujiunga katika klabu hiyo pamoja na mshambuliaji wa zamani wa Paris St-Germain Edinson Cavani, mwenye umri wa miaka 33.
Mkurugeni wa mchezi wa Lyon Juninho amefichua kuwa kiungo wa kati Houssem Aouar anaweza kuondoka katika klabu hiyo ya Ufaransa msimu huu, huku Arsenal, Manchester City na Juventus zote zikimfuatilia Mfaransa huyo mwenye umri wa miaka 22.
Tetesi zinasema West Bromwich Albion na Fulham wanakimbia kusaini mkataba na mshambuliaji wa Peterborough Muingereza Ivan Toney, mwenye umri wa miaka 24.
Juventus wamewasiliana na Arsenal juu ya uwezekano wa kumhamisha mshambuliaji Mfaransa Alexandre Lacazette, mwenye umri wa miaka 29.

Tetesi zinasema Arsenal wako makini sana kusaini mkataba na mchezaji mwenye umri wa miaka 17 anayechezea timu ya Sporting Lisbon 17- Joelson Fernandes.
Mshambuliaji huyo amepewa jina la ‘Cristiano Ronaldo mpya’ na the Gunners wanaweza kutoa ofa ya pesa na hata kuwatoa wachezaji wake ili kupata saini .
Tetesi zinasema Kiungo wa kati Mfaransa Paul Pogba, mwenye umri wa miaka 27, anaitarajia Manchester United ifungue mazungumzo ya mkataba pale michuano ya Ligi ya Europa itakapokamilika.
Tottenham wako tayari kuwaruhusu viungo wa kati -Waingereza Oliver Skipp mwenye umri wa miaka 19 na Jamie Bowden kuondoka kwa deni baada ya kusaini mkataba na Dane Pierre-Emile Hojbjerg, mwenye umri wa miaka 25, kutoka Southampton.

Atletico Madrid wamemtaja golikipa wa timu ya Eibar Mserbia Marko Dmitrovic, mwenye umri wa miaka 28, kuwa ndiye mlindalango wa kwanza wanayemlenga katika kipindi cha dirisha la uhamisho, ili kuwa na mlindalango wa akiba baada ya Mslovenia Jan Oblak kuhusishwa na Chelsea.
Leicester City ni moja ya klabu zinazohusishwa na uhamisho wa winga wa Bournemouth mwenye umri wa miaka 23- David Brooks – lakini bosi mpya wa Cherries Jason Tindall anasisitiza kuwa hakutakuwa na “mauzo ya makubwa ” ya wachezaji nyota wa klabu .
Velez Sarsfield wanania ya kumnunua mshambuliaji wa safu ya kati wa Southampton Muargentina Guido Carrillo, 29.
Meneja wa timu ya Manchester United ya vijana walio chini ya miaka 23 Neil Wood amesisistiza kuwa Mfaransa Hannibal Mejbri anayecheza safu ya kati ya vijana walio chini ya miaka ,17, atasalia katika sehemu ya timu ya vijana inayopangwa kwa ajili ya msimu ujao .
Umekuwa mteja muaminifu wa meridianbet? Basi fahamu kuwa kuna zawadi kibao hadi 5% ya pesa yako inarejeshwa kwako. Kila wiki unaweza kurudishiwa mpaka Tsh 250,000.


rama
Maoni:man city waitaji kiungo pale kati katikati pale hawako vizuri sana
Mwajumah
Asante kwa taarifa#Meridianbettz
Sauda
Makala safi!!!
Nasra
Gud news
Adelta
Ni kwamba west bromwish,Albion na Fulham walikimbilia kusaini mkataba wa
Wa mshambuliaji @meridianbettz
Ester jackson
Itakuwa vizuri sana arsenal kupata saini ya kijana mdogo sana mwenye umri wa chini kabisa 17 wenye uwezo wa Jina la Christian ronaldo
Latifa juma mohamed
Habari njema
Zeiyana
Itakua vizuri joelson fenandes atazina pengo la Alexander kama husajiri ukimilka kwenda juventus
Khadija
Habari njema#meridianbettz
Njiku
Ipo poa sana hii good news
aisha
Manchester city watafanya vizuri sana wakimpata kiungo huyo
neema hassan
Asante kwa taarifa
Sadick
Bado sijaona pilika pilika makini za usajiri zaidi ya maneno ya hapa na pale#meridianbettz
Lydia Emmanuel Magoti
Wachambuzi mpo vizuri kwa hili
Venerose
Asante kwa taarifa
Ernest
Vertonghen deal jeupe kwenda Benfica
Rehema
Habari njema
Salma ngende
Habari nzuri
Samiah
Nice
farida ahmadi
Habari nzuri kwa mashabiki wa Manchester city
Caroline
Asante meridianbet Kwa taarifa
Povel
Gud
Fatuma kasomo
Habari njema
Furahav
Msimu ujao itakua noma sana.
Gabriel
Usajili uko vzur sana
Saupha mohamed
Good
Devotha
Good update
Asia Abdy
Nice
Sabrina
Man u wanatamaa kila sehemu wanapigania wao
Janeflora malisa
Vzr
Dorophina
Man City inatakiwa iongeze usajili kwa sasa bado hawajakamilisha kikosi cha kati
magdalena
mambo yanazidi kupamba moto dirisha la usajili katika vilabu mbalimbali
felister
usajili umepamba moto
Rose kapinga
Mambo yanazidi kua mazuri!!!
Tatu
Good news
Hope mwaikuka
Taarifa imeeleweka
David Pere
Bado sijaona pilika pilika makini za usajiri zaidi ya maneno ya hapa na pale
warda
City wakimpata huyu wamelamba dodo
Shafii
Tetesi ziko vizuri Sana hapo kazi kwa makocha kupigana vikumbo sokoni.