Ivan Toney amekashifu uvumi unaoendelea na kusumbua juu ya lengo la Shirikisho la Soka (FA) kufungiwa kwa madai yake ya kukiuka sheria za kamari.
Mshambuliajii huyo wa Brentford ameshtakiwa kwa makosa 262 ya ukiukaji wa sheria na bodi inayosimamia soka la Uingereza, ambayo ilifanyika kwa kipindi cha miaka minne lakini pia hakujawa na taarifa rasmi za FA kuhusu suala hilo ripoti hapo awali na Daily Mail Jumanne, zilidai Toney amekiri mashtaka mengi na anaweza kupigwa marufuku kwa miezi sita.
Ripoti hizo zilionyesha kuwa kijana huyo mwenye umri wa miaka 26 pia amekanusha baadhi ya ukiukaji huo, ingawa Toney ameshangazwa na uvujaji ulioripotiwa ndani ya FA.
Aliandika kwenye Instagram hapo jana: “Nilishtushwa na kusikitishwa kuona uvumi kutoka kwa waandishi wa habari jana na leo kuhusu mchakato wa uchunguzi wa FA unaonihusu baada ya kuambiwa na FA kuwa ni mchakato wa siri hadi uamuzi wowote utakapofanywa.”
Inasikitisha sana kwangu kusoma kwamba FA inasema nitafungiwa kucheza soka kwa muda wa miezi sita kabla hata kusikilizwa kwa kesi na inanifanya niwe na wasiwasi kuhusu mchakato huo. Alisema mchezaji huyo.
Toney aliitwa kwa mara ya kwanza Uingereza mwezi Septemba lakini aliachwa nje ya kikosi cha Gareth Southgate kwa Kombe la Dunia. Mtendaji mkuu wa FA Mark Bullingham alisema kuwa kukosekana kwa mshambuliaji huyo kwenye kikosi cha Qatar kuliamuliwa kwa msingi wa soka.
Toney anapanga kupinga FA baada ya tukio la pili la uvujaji ulioripotiwa.
Aliongeza: “Mawakili wangu watakuwa wakiandikia FA kuomba wafanye uchunguzi wa uvujaji, kwani hii ni mara ya pili kwa habari kutoka kwenye magazeti na mara ya mwisho ilikuwa kabla ya uteuzi wa kikosi cha Kombe la Dunia la Uingereza.”
Toney amesema kuwa anapoendelea kuambiwa uchunguzi unakusudiwa kuwa siri, hawezi kutoa maon yoyote zaidi na ataendelea kuzingatia soka lake.